Saturday, January 5, 2013

HATUA ZA KUJUA PENZI LINAPOTEZA UELEKEO


HATUA ZA KUJUA PENZI LINAPOTEZA UELEKEO.

Hatua kuu zinazoonyesha penzi limepoteza uelekeo ni hizi hapa:-
1.      MAWASILIANO KUWA DUNI
2.      USO KUONESHA KUWA HAPENDI KUONGEA
3.      HASIRA ZA MARA KWA MARA
4.      MANENO YASIYOFAA HUANZA KUZUNGUMZWA
5.      KUDAI KUTENGANA

 

1. MAWASILIANO KUWA DUNI

Mapenzi na sawa na jani la mti. Huendelea kuwa na mawasiliano na shina kwa kusaidiana na matawi. Ila siku ikifika jani linadondoka. Hii utokea pale jani linapochoka na maisha ya kujishikiza. Haya ndiyo sawa yalio kwetu binadamu. Mwanzo uanza kwa kasi zaidi na mwisho hufifia kwa mawasiliano. Mtu anaweza kukata mawasiliano kwa sababu zake binafsi zikiwemo hizo za hapo juu.

Kama mawasiliano yalikuwa ni mara tano kwa siku (kwa wale walio mbali, mfano masomoni.), basi mawasiliano yanaaza kushuka hadi mara mbili hadi mwisho wa siku mawasiliano kukaka kabisa. Hapa kila mmoja akiulizwa swali kwanini husema nilibanwa na kazi ndio maana sikuweza kukutafuta.
Kwa walio kwenye ndoa mawasiliano pia yanakuwa nyuma kidogo. Kama alikuwa anakusalimia kwa kukumbatiana, hapa hali hua tofauti kabisa. Muda mwingine kila mtu na kazi yake. Kila mtu shuka yake, na kukicha kila mtu kivyake.

Hii hua na athari sana pale mmoja wa wapenzi anapokuwa na mpenzi mwingine. Yule ambaye ulidhani umemchagua anakuja kuwa sumu kwako. Unapenda umwone yeye ataki. Unapenda umpe zawadi yeye ataki, unapenda kutoka naye out yeye ataki, na pale anaposema uwasiliane naye basi roho huweka pembeni. Utagundua kuwa kama analazimishwa aongee.

Ikifikia sehemu hii na kama ulimpenda kweli basi utaongeza jitihada za kutaka kuwa naye, wasio na imani hufikia mahali wanasema nitaendelea kukaa bila kuoa. Kauli hii ni udanganyifu tu. Akisahau yale yaliyomtokea, anaamua kusaka mke au mume mwingine. Unapoona hali hii imeanza jalibu kuwajilazimisha kuwa karibu yake sana. Na pale unavyoona hali ni mbaya zaidi basi mweleze rafiki yake wa karibu ambaye humwamini kwa kila jambo.

Au unaweza kumweleza mtu anayeheshimika ili asikilize kilio chako na mwisho wa siku utaona mafanikio. Hii ni kwa wachumba na hata kwa wanandoa itapotakiwa kufanya hili.

Kwa wanandoa ni muhimu wawaone pia wezee wa busara ambao wanaaminika na kukubalika na jamii. Ikishindikana basi waende katika ofisi ya kata au ustawi wa jamii kwa msaada zaidi.

 

 

2. USO HUONYESHA KUWA HAPENDI KUONGEA

Ni hali ya kawaida kuona mke au mme kuonyesha kuwa apendi kuongea na wewe. Sababu kubwa anayo moyoni na hataki kuisema. Uso mara nyingi unakuwa na asili ya mkunjo kwa wanawake. Na kwa wanaume sura inakuwa na asili na makunyanzi. Hapo ujue kuwa hali ni mbaya sana. Hapo hata ukimsesha anaona kama unajisumbua tuu. Na kama ataamua kusema ni kidogo tu na mwisho inaedelea kukaa kimwa.

Pia hata majibu yake uteyaelewa tu. Ni ya unyonge hivi, na sauti ya chini isiyo na mvuto au ushawishi kwa mwenzake. Pakifikia mahali kama hapa jalibu kumnunulia zawadi mzuri, kumkisi, kumwambia oooo mpenzi wangu….nakupenda sana…….leo umependeza namna hii….. Kweli mimi nimechagua mke mzuri au mme mzuri sana……kwani najivunia sana kukuona na kuwa na wewe muda wote.

Wakati mwingine unaweza kwenda kumsaidia kupika, kuosha vyombo na hata kumwambia mkaoge pamoja. Utaona jinsi anavyoanza kubadilika mpenzi wako. Hapa hakuna mchawi bali ni namna tabia yako ulivyomwonyesha. Hali hii haiwezi kwisha ghafla kama kimbunga bali huenda taratibu na mwisho wa siki hali inajirudia. Kwa hali ya kawaida uchukua kuanzia siku 21-22. Uendelea kumwambia maneno yenye baraka na busara bila ya kukata tama. Uwe na imanii ya hali ya juu kwani majibu utayokutana nayo si ya kawaida, lakini mwisho wa siku hali itarudi kuwa ya kawaida kabisa.

 

                                   3. HASIRA ZA MARA KWA MARA.

Hatua hii mpenzi wako huanza kuchukia kila jambo. Utende mema yeye kwake ni baya. Utajiongelesha ni kama unamuongezea hasira. Hapa ndipo watu huwa wanafikia kuchukua hatua ya kujiua wenyewe kisa mpenzi wake amamsaliti. Mfano wa majibu utayokutana nayo ni kama haya:-
  1. mbona hivi mpenzi?
  2. mimi nifanyaje?
Wewe yanakuhusu nini?
Umepata hasara gani mimi kufanya hivi?
Fanya utakavyo?
Mimi ndo kila kitu?
  1. kwa nini yamefikia hapo?
  2. we ujui?
Hizi ni baadhi ya changamoto utazokutana nazo wakati wa maojiano yako na mpenzi wako. Usimpige kisa majibu ya mkato. Kama mwanaume hali ikizidi kuwa ni kelele tu, basi kaa kimya au ondoka na kwenda kufanya shughuli zingine. Utavyorudi atashindwa anzie wapi.

Kama ni upande wa mwanamke yanamtokea haya basi fanya hivi:- kaa kimya kwa muda, atakaa kimya mpenzi wako. Kasha usisite kumwandalia mmeo chakula cha kutosha na kizuri. Hata kama hali usichoke kuandaa. Mpe maneno matamu mkiwa kitandani na kujaribu kumgusagusa sehemu mbalimbali za mwili. Hapa mwanaume ujanja unaisha hapo.

Kama hizo njia zinachukuwa muda mrefu basi anza kwa kumuomba msamaha. Hata kumpigia magoti usione aibu. Piga huku ukionyeshwa kuwa hali hile upendezwi nayo. Ni ya bahati mbaya. Hakirudi katika hali ya kawaida na siku nyingi kupita anza kushusha makombola kwa njia ya utani kuwa pale mme wangu kosa lilikuwa lako. Kama muelewa ataweza kijirekebisha ipasavyo na mwisho wa siku mukarudi kama siku ya kwanza kuanza penzi lenu.

 

4. MANENO YASIYOFAA HUANZA KUZUNGUMZWA

Hii ni hatua ya nne ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu. Mpenzi wako hutamuona mchungu kupita kiasi. Hutaona kama kuna watu wanamfundisha kuongea maneno haya. Ukweli ni kwamba ukishaona mke wako mara nyingi yeye na wenzake, hana muda wa kukaa akuandalie chakula (kwa mwanamke aliye kwenye ndoa) basi ujue kwamba rafiki zake wamemfundisha na ujue kuna jambo linaendelea ambolo mwisho wake ni kutengana.

Kwa mchumba basi utaona maneno ya ovyo ovyo ili mradi umwambie sasa mimi na wewe basi. Atafanya kila aina awezavyo utengane. Hii huweza kuwa mwanaumme ndio kisa au mke mwenyewe ndio kisa. Akishindwa hapa anaamua kuchukuwa maamuzi magumu sana ambayo hutasahau tena maishani. Kama vile kumpigia mpenzi wake mpya na kuanza kuongea naye.

Hiyo atakuwa amekuheshimu, anamkumbatia na kumkiss ili mradi uhuzunike kwa hili kasha mtenge ili awe huru. Hali hii huwa ni mbaya zaidi kama mtu umependa. Hhiki ni sawa na wanavyofanya wanaume walio wengi katika uchumba na doa. Ukimuuliza namba hii uliyosevu Juma mbona inaonyesha ni hile ya Asha atakuambia ni rafiki yangu.

Ukiendelea kumbana atakuambia ni ya mke wangu. Sasa wewe unasemaje au unataka nini? Haya utokea kwa wote wenye ndoa zao na wale walio kwenye uchumba bila kujali mme au mke au mchumba.Haya ndiyo yanayojili sehemu hii iwapo utashindwa kutatua hizo hatua tatu za mwanzo.

Namna ya kutatua sehemu hii ni kutumia zile njia elekezi ya hatua ya kwanza. Kubwa zaidi hapa ni kuomba msamaha kwa kile kinachovumilika, na kile ambacho akivumiliki ni kwenda kwa washauri nasaha kama vile maafisa ustawi wa jamii kwa manufaa ya wote. Wao watakusaidia vizuri hata kama uko peke yako na mwenza wako alikataa kwenda huko. Utamsahau na kuiona dunia ni tamu zaidi y asana na utasema mwenyewe ulichelewa wapi kipindi yanatokea haya.

 

                           5. KUDAI KUTENGANA

Kama mnavyojua, mti uota, ukua, utengeneza majani, huishi na hatimae mwisho kufa. Hapa mpenzi wako utaona ni balaa tupu. Yaani hafai hata kidogo. Kama una imani ndogo utatamani uondoke uende mbali ambako hutamwona tena. Hapa hakuna jinsi, hata mahakama huamua kutenganisha ndoa kama walioana. Hapa usipofanya kama atakavyo mpenzi wako unaweza kuishia hata gerezani au kuchukua uamuzi wa kumpiga.

Kweli inauma sana kumwona mke/mme au mchumba unaempendaanataka mutengane. Wengine huamua kujinyonga, wengine kunywa sumu, wengine wanaamia baa na kuweka makazi yao. Mmoja hakikataa hakuna jinsi, mwache aende kwa usalama.

Jinsi ya kutatua hili ni kwamba unapaswa kwenda kukubali tatizo lililotokea. Kwani kinachotokea kwa wenzako hata wewe ipo siku yatatokea. Katika maisha ya binadamu kuna kupenda na kutendwa, hivyo kutengana ni moja ya sehemu ya maisha. Jaribu kutembelea sehemu zenye mkusanyiko wa watu. Lakini usinywe pombe, na kama ulikuwa unakunya unaweza kuacha kabisa hatakwa miezi kadha na usitembelee sehemu za pombe.

Unaweza kwenda disco na sehemu nyinginezo mzuri kama vile kwenye mpira, kucheza puru, drafti, bao na hata karata. Hali yako itarudi kama zamani. Utajiona wa kawaida (hii ni kama kwa mwanaume). Ukikutana naye usimwone kama ni adui ako mkubwa, kwani yaliyotokea ni majaribu ya dunia. Na pale mkaapo kwa muda mrefu na kuona kuna umuhimu wa kurudiana basi murudiane kwa moya mmoja.

Kwa wanawake huchukua muda mrefu kama tendo lilifanywa na mwanaume. Na tatizo lenyewe kama kumfumania mme au mchumba wake wakiwa katika chumba kile kile anacholala yeye. Huwa anaona ni unyama. Kwa hili, mke huyu kurudiana naye itachukua muda mwingi kwani lile swala humrudia mara kwa mara. Na kama alimpenda sana bwana wake huamua usikuone kamwe.

Lakini hakuna jambo lisilo na mwisho. Mme unapaswa kwenda kuomba msamaha kwa yule mke wako uliyemwacha. Kukataliwa kwa mara ya kwanza ni jambo la kawaida, kwani ile icha itaendelea kumrudia. Jifanye kama usikii, fanya hivi zaidi ya mara tano hadi kumi. Mke wako au mme wako ataanza kukuonea huruma na hatimae kuwa naye pamoja.
NB: ieleweke kwamba si kila unayemfanyia tukio baya ataweza kukusamehe. Ni wachache wenye nyoyo kama hizo. Bora ubadilike na kutunza utu na uthamani wako mapema. Kwa kufanya hili maisha utayaona kama maji ya kunywa.


No comments:

Post a Comment